87 - AL - AA'LAA |
| |
|
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. |
| |
| |
| 1 | Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa, |
| |
| 2 | Aliye umba, na akaweka sawa, |
| |
| 3 | Na ambaye amekadiria na akaongoa, |
| |
| 4 | Na aliye otesha malisho, |
| |
| 5 | Kisha akayafanya makavu, meusi. |
| |
| 6 | Tutakusomesha wala hutasahau, |
| |
| 7 | Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana. |
| |
| 8 | Na tutakusahilishia yawe mepesi. |
| |
| 9 | Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa. |
| |
| 10 | Atakumbuka mwenye kuogopa. |
| |
| 11 | Na atajitenga mbali nayo mpotovu, |
| |
| 12 | Ambaye atauingia Moto mkubwa. |
| |
| 13 | Tena humo hatakufa wala hawi hai. |
| |
| 14 | Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa. |
| |
| 15 | Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali. |
| |
| 16 | Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia! |
| |
| 17 | Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi. |
| |
| 18 | Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo, |
| |
| 19 | Vitabu vya Ibrahimu na Musa. |
| |