88 - AL - GHAASHIYAH |
| |
|
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. |
| |
| |
| 1 | Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza? |
| |
| 2 | Siku hiyo nyuso zitainama, |
| |
| 3 | Zikifanya kazi, nazo taabani. |
| |
| 4 | Ziingie katika Moto unao waka - |
| |
| 5 | Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka. |
| |
| 6 | Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba. |
| |
| 7 | Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa. |
| |
| 8 | Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu. |
| |
| 9 | Zitakuwa radhi kwa juhudi yao, |
| |
| 10 | Katika Bustani ya juu. |
| |
| 11 | Hawatasikia humo upuuzi. |
| |
| 12 | Humo imo chemchem inayo miminika. |
| |
| 13 | Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa, |
| |
| 14 | Na bilauri zilizo pangwa, |
| |
| 15 | Na matakia safu safu, |
| |
| 16 | Na mazulia yaliyo tandikwa. |
| |
| 17 | Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa? |
| |
| 18 | Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa? |
| |
| 19 | Na milima jinsi ilivyo thibitishwa? |
| |
| 20 | Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa? |
| |
| 21 | Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji. |
| |
| 22 | Wewe si mwenye kuwatawalia. |
| |
| 23 | Lakini anaye rudi nyuma na kukataa, |
| |
| 24 | Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa! |
| |
| 25 | Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao. |
| |
| 26 | Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao! |
| |