91 - ASH-SHAMS |
| |
|
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. |
| |
| |
| 1 | Naapa kwa jua na mwangaza wake! |
| |
| 2 | Na kwa mwezi unapo lifuatia! |
| |
| 3 | Na kwa mchana unapo lidhihirisha! |
| |
| 4 | Na kwa usiku unapo lifunika! |
| |
| 5 | Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga! |
| |
| 6 | Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza! |
| |
| 7 | Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza! |
| |
| 8 | Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake, |
| |
| 9 | Hakika amefanikiwa aliye itakasa, |
| |
| 10 | Na hakika amekhasiri aliye iviza. |
| |
| 11 | Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao, |
| |
| 12 | Alipo simama mwovu wao mkubwa, |
| |
| 13 | Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake. |
| |
| 14 | Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa. |
| |
| 15 | Wala Yeye haogopi matokeo yake. |
| |