101 - AL - QAARIA'H |
| |
|
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. |
| |
| |
| 1 | Inayo gonga! |
| |
| 2 | Nini Inayo gonga? |
| |
| 3 | Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga? |
| |
| 4 | Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika; |
| |
| 5 | Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa! |
| |
| 6 | Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, |
| |
| 7 | Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza. |
| |
| 8 | Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, |
| |
| 9 | Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya! |
| |
| 10 | Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo? |
| |
| 11 | Ni Moto mkali! |
| |