___Translations___

_Quran?_

_Gadgets_

_Search_

_Links_

_Contribute_

_Note_

1 - AL-FAATIH'A
2 - AL - BAQARA
3 - AL I'MRAN
4 - AN-NISAAI
5 - AL - MAIDA
6 - AL - AN-A'AM
7 - AL - A'RAAF
8 - AL - ANFAAL
9 - AT-TAWBA
10 - YUNUS
11 - HUD
12 - YUSUF
13 - AR-RAA'D
14 - IBRAHIM
15 - AL - HIJR
16 - AN NAH'L
17 - AL ISRAAI (BANI ISRAIL)
18 - AL - KAHF
19 - MARYAM
20 - T'AHA
21 - AL - ANBIYAA
22 - AL -HAJJ
23 - AL - MUUMINUN
24 - AN - NUR
25 - AL - FURQAN
26 - ASH-SHUA'RAA
27 - AN-NAML
28 - AL-QAS'AS'
29 - AL - A'NKABUT
30 - AR-RUM
31 - LUQMAN
32 - ASSAJDAH
33 - AL-AH'ZAB
34 - SABAA
35 - FAAT'IR
36 - YA-SIN
37 - ASS'AFFAT
38 - S'AAD
39 - AZZUMAR
40 - GHAAFIR (AU AL MUUMIN)
41 - FUSS'ILAT (AU H'A MIM SAJDAH)
42 - ASH-SHUURA
43 - AZZUKHRUF
44 - ADDUKHAN
45 - AL - JAATHIYA
46 - AL - AH'QAAF
47 - MUH'AMMAD
48 - AL FAT-H'I
49 - AL H'UJURAAT
50 - QAAF
51 - ADH-DHAARIYAAT
52 - ATT'UR
53 - ANNAJM
54 - AL-QAMAR
55 - ARRAH'MAN
56 - AL -WAAQIA'H
57 - AL -H'ADIID
58 - AL - MUJAADALAH
59 - AL - H'ASHRI
60 - AL - MUMTAH'INAH
61 - ASS'AF
62 - AL - JUMUA'
63 - AL - MUNAAFIQUN
64 - ATTAGHAABUN
65 - ATT'ALAAQ
66 - ATTAH'RIIM
67 - AL - MULK
68 - AL - QALAM
69 - AL - H'AAQQAH
70 - AL - MAA'RIJ
71 - NUH'
72 - AL - JINN
73 - AL - MUZZAMMIL
74 - AL - MUDDATHTHIR
75 - AL - QIYAMAH
76 - AL - INSAN
77 - AL - MURSALAAT
78 - ANNABAA
79 - ANNAZIA'AT
80 - A'BASA
81 - ATTAKWIR
82 - AL - INFIT'AAR
83 - AL - MUT'AFFIFIIN
84 - AL - INSHIQAAQ
85 - AL - BURUUJ
86 - ATT'AARIQ
87 - AL - AA'LAA
88 - AL - GHAASHIYAH
89 - AL - FAJR
90 - AL - BALAD
91 - ASH-SHAMS
92 - AL - LAYL
93 - WADH-DHUH'AA
94 - ASH-SHARH'
95 - AT-TIN
96 - AL - A'LAQ
97 - AL - QADR
98 - AL - BAYYINAH
99 - AZ-ZILZALAH
100 - AL - A'ADIYAAT
101 - AL - QAARIA'H
102 - AT-TAKAATHUR
103 - AL - A'S'R
104 - AL - HUMAZAH
105 - AL - FIIL
106 - QURAISH
107 - AL - MAAU'N
108 - AL - KAWTHAR
109 - AL - KAFIRUN
110 - ANNAS'R
111 - AL - MASAD
112 - AL - IKHLAS'
113 - AL - FALAQ
114 - ANNAS
KISWAHILI

37 - ASS'AFFAT

 

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
 
2Na kwa wenye kukataza mabaya.
 
3Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
 
4Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
 
5Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
 
6Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
 
7Na kulinda na kila shet'ani a'si.
 
8Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
 
9Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
 
10Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
 
11Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
 
12Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
 
13Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
 
14Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
 
15Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
 
16Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
 
17Hata baba zetu wa zamani?
 
18Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
 
19Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
 
20Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
 
21Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
 
22Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
 
23Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
 
24Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
 
25Mna nini? Mbona hamsaidiani?
 
26Bali hii leo, watasalimu amri.
 
27Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
 
28Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
 
29Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
 
30Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
 
31Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
 
32Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
 
33Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
 
34Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
 
35Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
 
36Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
 
37Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
 
38Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
 
39Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
 
40Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
 
41Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
 
42Matunda, nao watahishimiwa.
 
43Katika Bustani za neema.
 
44Wako juu ya viti wamekabiliana.
 
45Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
 
46Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
 
47Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
 
48Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
 
49Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
 
50Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
 
51Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
 
52Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
 
53Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
 
54Atasema: Je! Nyie mnawaona?
 
55Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
 
56Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
 
57Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
 
58Je! Sisi hatutakufa,
 
59Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
 
60Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
 
61Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
 
62Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
 
63Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
 
64Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
 
65Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
 
66Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
 
67Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
 
68Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
 
69Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
 
70Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
 
71Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
 
72Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
 
73Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
 
74Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
 
75Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
 
76Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
 
77Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
 
78Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
 
79Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
 
80Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
 
81Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
 
82Kisha tukawazamisha wale wengine.
 
83Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
 
84Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
 
85Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
 
86Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
 
87Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
 
88Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
 
89Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
 
90Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
 
91Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
 
92Mna nini hata hamsemi?
 
93Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
 
94Basi wakamjia upesi upesi.
 
95Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
 
96Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
 
97Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
 
98Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
 
99Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
 
100Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
 
101Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
 
102Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
 
103Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
 
104Tulimwita: Ewe Ibrahim!
 
105Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
 
106Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
 
107Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
 
108Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
 
109Iwe salama kwa Ibrahim!
 
110Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
 
111Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
 
112Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
 
113Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
 
114Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
 
115Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
 
116Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
 
117Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
 
118Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
 
119Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
 
120Iwe salama kwa Musa na Haruni!
 
121Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
 
122Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
 
123Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
 
124Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?
 
125Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
 
126Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
 
127Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
 
128Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
 
129Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
 
130Iwe salama kwa Ilyas.
 
131Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
 
132Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
 
133Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
 
134Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
 
135Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
 
136Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
 
137Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
 
138Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?
 
139Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
 
140Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
 
141Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
 
142Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
 
143Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
 
144Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
 
145Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
 
146Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
 
147Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
 
148Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
 
149Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
 
150Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
 
151Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
 
152Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
 
153Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
 
154Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
 
155Hamkumbuki?
 
156Au mnayo hoja iliyo wazi?
 
157Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
 
158Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
 
159Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
 
160Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
 
161Basi hakika nyinyi na mnao waabudu
 
162Hamwezi kuwapoteza
 
163Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.
 
164Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
 
165Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
 
166Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
 
167Na walikuwapo walio kuwa wakisema:
 
168Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
 
169Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
 
170Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
 
171Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
 
172Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
 
173Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
 
174Basi waachilie mbali kwa muda.
 
175Na watazame, nao wataona.
 
176Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
 
177Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
 
178Na waache kwa muda.
 
179Na tazama, na wao wataona.
 
180Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
 
181Na Salamu juu ya Mitume.
 
182Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.