___Translations___

_Quran?_

_Gadgets_

_Search_

_Links_

_Contribute_

_Note_

1 - AL-FAATIH'A
2 - AL - BAQARA
3 - AL I'MRAN
4 - AN-NISAAI
5 - AL - MAIDA
6 - AL - AN-A'AM
7 - AL - A'RAAF
8 - AL - ANFAAL
9 - AT-TAWBA
10 - YUNUS
11 - HUD
12 - YUSUF
13 - AR-RAA'D
14 - IBRAHIM
15 - AL - HIJR
16 - AN NAH'L
17 - AL ISRAAI (BANI ISRAIL)
18 - AL - KAHF
19 - MARYAM
20 - T'AHA
21 - AL - ANBIYAA
22 - AL -HAJJ
23 - AL - MUUMINUN
24 - AN - NUR
25 - AL - FURQAN
26 - ASH-SHUA'RAA
27 - AN-NAML
28 - AL-QAS'AS'
29 - AL - A'NKABUT
30 - AR-RUM
31 - LUQMAN
32 - ASSAJDAH
33 - AL-AH'ZAB
34 - SABAA
35 - FAAT'IR
36 - YA-SIN
37 - ASS'AFFAT
38 - S'AAD
39 - AZZUMAR
40 - GHAAFIR (AU AL MUUMIN)
41 - FUSS'ILAT (AU H'A MIM SAJDAH)
42 - ASH-SHUURA
43 - AZZUKHRUF
44 - ADDUKHAN
45 - AL - JAATHIYA
46 - AL - AH'QAAF
47 - MUH'AMMAD
48 - AL FAT-H'I
49 - AL H'UJURAAT
50 - QAAF
51 - ADH-DHAARIYAAT
52 - ATT'UR
53 - ANNAJM
54 - AL-QAMAR
55 - ARRAH'MAN
56 - AL -WAAQIA'H
57 - AL -H'ADIID
58 - AL - MUJAADALAH
59 - AL - H'ASHRI
60 - AL - MUMTAH'INAH
61 - ASS'AF
62 - AL - JUMUA'
63 - AL - MUNAAFIQUN
64 - ATTAGHAABUN
65 - ATT'ALAAQ
66 - ATTAH'RIIM
67 - AL - MULK
68 - AL - QALAM
69 - AL - H'AAQQAH
70 - AL - MAA'RIJ
71 - NUH'
72 - AL - JINN
73 - AL - MUZZAMMIL
74 - AL - MUDDATHTHIR
75 - AL - QIYAMAH
76 - AL - INSAN
77 - AL - MURSALAAT
78 - ANNABAA
79 - ANNAZIA'AT
80 - A'BASA
81 - ATTAKWIR
82 - AL - INFIT'AAR
83 - AL - MUT'AFFIFIIN
84 - AL - INSHIQAAQ
85 - AL - BURUUJ
86 - ATT'AARIQ
87 - AL - AA'LAA
88 - AL - GHAASHIYAH
89 - AL - FAJR
90 - AL - BALAD
91 - ASH-SHAMS
92 - AL - LAYL
93 - WADH-DHUH'AA
94 - ASH-SHARH'
95 - AT-TIN
96 - AL - A'LAQ
97 - AL - QADR
98 - AL - BAYYINAH
99 - AZ-ZILZALAH
100 - AL - A'ADIYAAT
101 - AL - QAARIA'H
102 - AT-TAKAATHUR
103 - AL - A'S'R
104 - AL - HUMAZAH
105 - AL - FIIL
106 - QURAISH
107 - AL - MAAU'N
108 - AL - KAWTHAR
109 - AL - KAFIRUN
110 - ANNAS'R
111 - AL - MASAD
112 - AL - IKHLAS'
113 - AL - FALAQ
114 - ANNAS
KISWAHILI

75 - AL - QIYAMAH

 

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
 
2Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
 
3Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
 
4Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
 
5Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
 
6Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
 
7Basi jicho litapo dawaa,
 
8Na mwezi utapo patwa,
 
9Na likakusanywa jua na mwezi,
 
10Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
 
11La! Hapana pa kukimbilia!
 
12Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
 
13Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
 
14Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
 
15Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
 
16Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
 
17Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
 
18Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
 
19Kisha ni juu yetu kuubainisha.
 
20Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
 
21Na mnaacha maisha ya Akhera.
 
22Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
 
23Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
 
24Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
 
25Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
 
26La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
 
27Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
 
28Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
 
29Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
 
30Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
 
31Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
 
32Bali alikanusha, na akageuka.
 
33Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
 
34Ole wako, ole wako!
 
35Kisha Ole wako, ole wako!
 
36Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
 
37Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
 
38Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
 
39Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
 
40Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?