___Translations___

_Quran?_

_Gadgets_

_Search_

_Links_

_Contribute_

_Note_

1 - AL-FAATIH'A
2 - AL - BAQARA
3 - AL I'MRAN
4 - AN-NISAAI
5 - AL - MAIDA
6 - AL - AN-A'AM
7 - AL - A'RAAF
8 - AL - ANFAAL
9 - AT-TAWBA
10 - YUNUS
11 - HUD
12 - YUSUF
13 - AR-RAA'D
14 - IBRAHIM
15 - AL - HIJR
16 - AN NAH'L
17 - AL ISRAAI (BANI ISRAIL)
18 - AL - KAHF
19 - MARYAM
20 - T'AHA
21 - AL - ANBIYAA
22 - AL -HAJJ
23 - AL - MUUMINUN
24 - AN - NUR
25 - AL - FURQAN
26 - ASH-SHUA'RAA
27 - AN-NAML
28 - AL-QAS'AS'
29 - AL - A'NKABUT
30 - AR-RUM
31 - LUQMAN
32 - ASSAJDAH
33 - AL-AH'ZAB
34 - SABAA
35 - FAAT'IR
36 - YA-SIN
37 - ASS'AFFAT
38 - S'AAD
39 - AZZUMAR
40 - GHAAFIR (AU AL MUUMIN)
41 - FUSS'ILAT (AU H'A MIM SAJDAH)
42 - ASH-SHUURA
43 - AZZUKHRUF
44 - ADDUKHAN
45 - AL - JAATHIYA
46 - AL - AH'QAAF
47 - MUH'AMMAD
48 - AL FAT-H'I
49 - AL H'UJURAAT
50 - QAAF
51 - ADH-DHAARIYAAT
52 - ATT'UR
53 - ANNAJM
54 - AL-QAMAR
55 - ARRAH'MAN
56 - AL -WAAQIA'H
57 - AL -H'ADIID
58 - AL - MUJAADALAH
59 - AL - H'ASHRI
60 - AL - MUMTAH'INAH
61 - ASS'AF
62 - AL - JUMUA'
63 - AL - MUNAAFIQUN
64 - ATTAGHAABUN
65 - ATT'ALAAQ
66 - ATTAH'RIIM
67 - AL - MULK
68 - AL - QALAM
69 - AL - H'AAQQAH
70 - AL - MAA'RIJ
71 - NUH'
72 - AL - JINN
73 - AL - MUZZAMMIL
74 - AL - MUDDATHTHIR
75 - AL - QIYAMAH
76 - AL - INSAN
77 - AL - MURSALAAT
78 - ANNABAA
79 - ANNAZIA'AT
80 - A'BASA
81 - ATTAKWIR
82 - AL - INFIT'AAR
83 - AL - MUT'AFFIFIIN
84 - AL - INSHIQAAQ
85 - AL - BURUUJ
86 - ATT'AARIQ
87 - AL - AA'LAA
88 - AL - GHAASHIYAH
89 - AL - FAJR
90 - AL - BALAD
91 - ASH-SHAMS
92 - AL - LAYL
93 - WADH-DHUH'AA
94 - ASH-SHARH'
95 - AT-TIN
96 - AL - A'LAQ
97 - AL - QADR
98 - AL - BAYYINAH
99 - AZ-ZILZALAH
100 - AL - A'ADIYAAT
101 - AL - QAARIA'H
102 - AT-TAKAATHUR
103 - AL - A'S'R
104 - AL - HUMAZAH
105 - AL - FIIL
106 - QURAISH
107 - AL - MAAU'N
108 - AL - KAWTHAR
109 - AL - KAFIRUN
110 - ANNAS'R
111 - AL - MASAD
112 - AL - IKHLAS'
113 - AL - FALAQ
114 - ANNAS
KISWAHILI

74 - AL - MUDDATHTHIR

 

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Ewe uliye jigubika!
 
2Simama uonye!
 
3Na Mola wako Mlezi mtukuze!
 
4Na nguo zako, zisafishe.
 
5Na yaliyo machafu yahame!
 
6Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
 
7Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
 
8Basi litapo pulizwa barugumu,
 
9Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
 
10Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
 
11Niache peke yangu na niliye muumba;
 
12Na nikamjaalia awe na mali mengi,
 
13Na wana wanao onekana,
 
14Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
 
15Kisha anatumai nimzidishie!
 
16Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
 
17Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
 
18Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
 
19Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
 
20Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
 
21Kisha akatazama,
 
22Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
 
23Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
 
24Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
 
25Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
 
26Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
 
27Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
 
28Haubakishi wala hausazi.
 
29Unababua ngozi iwe nyeusi.
 
30Juu yake wapo kumi na tisa.
 
31Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.
 
32Hasha! Naapa kwa mwezi!
 
33Na kwa usiku unapo kucha!
 
34Na kwa asubuhi inapo pambazuka!
 
35Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!
 
36Ni onyo kwa binaadamu,
 
37Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.
 
38Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.
 
39Isipo kuwa watu wa kuliani.
 
40Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana
 
41Khabari za wakosefu:
 
42Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
 
43Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakisali.
 
44Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
 
45Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.
 
46Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.
 
47Mpaka yakini ilipo tufikia.
 
48Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
 
49Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
 
50Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
 
51Wanao mkimbia simba!
 
52Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
 
53Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
 
54Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
 
55Basi anaye taka atakumbuka.
 
56Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.